MARRIAGE WORKSHOP NA CHAKULA CHA JIONI

Marriage Workshop hiyo ilipambwa na mafundisho ya tofauti yakiongozwa wamtumishi wa Mungu, Mtume Onesmo Ndegi na Mwl Lilian Ndegi kuhusu watu walio katika Kristo Yesu maisha yao yanapaswa kuwa vipi,Usiku huo pia uliudhuliwa na watu mbalimbali wake kwa waume,pia mzazi mmoja mmoja,vijana walijitokeza kwa kiasi kikubwa kwa kile kilicho dhaniwa kuwa ni kupata mafundisho kwa ajili ya maandalizi ya maisha yao ya baadae kabla ya ndoa.

Jioni hiyo pia ilikuwa ni Marriage Anniversary ya Mtume Onesmo Ndegi na Mwl Lilian Ndegi hivyo usiku huo kulikuwa na kufungua Champagne pia kukata keki kwa ajili ya watumishi wa Mungu hao na chakula cha pamoja kwa wote.

Baadhi ya wanandoa walipata kuuliza maswali kuhusu changamoto wanazo kutana nazo katika ndoa.



Mtume Ndegi na Lilian Ndegi 

Wanandoa walioudhulia ndoa hiyo wakifuatilia mafundisho katika tukio hilo







Pastor Naomi Mhamba akitoa ushuhuda kuhusu Maisha yake ya Ndoa